Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Friday, 23 November 2012

Rais Muhammad Mursi akubali masharti ya Wazayuni

Rais Muhammad Mursi wa Misri amekubali mapendekezo yaliyotolewa na viongozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel la kuwekwa mifumo ya  elektroniki itakayolinda mipaka, ikiwa ni miongoni mwa masharti ya kukubali kusitisha mapigano kati ya utawala huo ghasibu na Wapalestina wa eneo la Ukanda wa Gaza. Taarifa zinasema kuwa, Hosni Mubarak dikteta wa zamani aliyeng'olewa madarakani nchini humo, kwa muda wa miongo mitatu  alikuwa akipinga vikali pendekezo hilo kwa kusema kuwa linainyima  Misri haki ya  kudhibiti kikamilifu mipaka yake. Duru za habari kutoka Tel Aviv zinasema kuwa, katika hali ambayo Rais Mursi amekubali pendekezo hilo, amma taasisi na asasi  za kisiasa na kiusalama za Israel haziamini kwamba kiongozi huyo wa Misri ataweza kutekeleza kikamilifu ahadi yake hiyo. Iwapo mifumo hiyo ya elektroniki itawekwa kwenye mipaka ya Misri na utawala wa Israel, majeshi ya utawala huo ghasibu yataweza kukusanya taarifa zote za kiusalama mpakani na kuzituma makao makuu ya jeshi la Israel.

0 comments:

Post a Comment