Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Friday, 16 November 2012

Qandil atembelea Ghaza kuunga mkono Wapalestina

Waziri Mkuu wa Misri, Hisham Qandil mapema leo amefanya ziara fupi katika ukanda wa Ghaza kwa lengo la kuonyesha uungaji mkono wake kwa wananchi wa Palestina hususan katika ukanda huo wanaoendelea kukabiliwa na mashambulizi ya utawala haramu wa Israel kwa siku ya tatu mfululizo. Qandil amelaani jinai hizo za Wazayuni dhidi ya wananchi wasio na hatia wa eneo la Ghaza na kusisitiza kuwa serikali ya Cairo haitafumbia macho mauaji hayo. Qandil ametembelea majeruhi wa Kipalestina katika hospitali moja huko Ghaza. Huku hayo yakijiri, Jumuiya ya Nchi zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote NAM imetoa taarifa ya kulaani mashambulizi ya Israel huko Ghaza na kulitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuchukua hatua za dharura kukomesha unyama huo wa Wazayuni.

0 comments:

Post a Comment