Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday, 15 November 2012

Mashambulizi ya Israeli huko Gaza hayakubaliki

Rais Muhammad Mursi wa Misri amesema kuwa, mashambulizi yanayofanywa na majeshi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika eneo la Ukanda wa Gaza, hayakubaliki hata kidogo. Rais Mursi amechukua uamuzi  wa kumrejesha nyumbani  balozi wa nchi hiyo aliyeko Tel Aviv, ikiwa ni radiamali ya kulalamikia unyama na ukatili unaofanywa na majeshi ya Israel dhidi ya wananchi wa Palestina wa eneo la Ukanda wa Gaza. Aidha Rais Mursi ametaka kiitishwe kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa shabaha ya kujadili mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza. Rais wa Misri amesisitiza kuwa, kushadidishwa mashambulizi hayo kutapelekea eneo la Mashariki ya Kati kukosa uthabiti. Kwa upande mwengine, Misri imefungua kivuko cha ardhini cha Rafah, baada ya kushadidi mashambulizi ya Wazayuni. Taarifa zinasema kuwa, kivuko hicho kimefunguliwa ili kuwaruhusu majeruhi wa Kipalestina kupelekwa kwenye hospitali ya al A'rish iliyoko upande wa Sinai ya Kaskazini ndani ya ardhi ya Misri. Inafaa kuashiria hapa kuwa, mashambulizi ya Wazayuni katika eneo hilo la Wapalestina yamesababisha watu wasiopungua 20 kuuawa shahidi na wengine zaidi ya 125 kujeruhiwa katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita

0 comments:

Post a Comment