Sikiliza Live
Sunday, 4 November 2012
Maalim Seif akemea kunyanyaswa Wazanzibari
Makamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ameelezea
kuchukizwa na vitendo vya unyanyasaji wa raia wasio na hatia
vilivyofanywa na Jeshi la Polisi likishirikiana na vikosi vya Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ). Maalim Seif Sharif Hamad ambaye pia ni
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF amevilaumu vyombo vya dola kwa
kutochukua hatua stahiki kudhibiti vitendo hivyo. Maalim Seif
amesisitiza kwamba, hatua zilizochukuliwa katika kurejesha amani baada
ya kutokea kwa vurugu hazikuwa sahihi, kwani zimekuwa zikiwadhalilisha
na kuwanyanyasa wananchi wasiokuwa na hatia pamoja na kuhujumu mali zao.
Katibu Mkuu huyo wa CUF ameeleza kuchukizwa pia na tukio la kuuawa kwa
askari polisi, Koplo Said Abdulrahmani, katika eneo la Bububu na
kuongeza kuwa, kuwa bado serikali na vyombo vya dola vina jukumu la
kulinda haki za raia kwa kuwasaka waliohusika na tukio hilo badala ya
kuwanyanyasa raia wasiokuwa na hatia. Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar ametahadharisha kuwa, huenda vitendo hivyo vimepangwa kuvuruga
umoja wa Wazanzibari na kuwataka wananchi kutokubali kuingizwa katika
mtego huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


0 comments:
Post a Comment