Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Sunday, 4 November 2012

UN yaonya kushambuliwa kijeshi nchi ya Mali

Umoja wa Mataifa umeonya kuhusiana na matokeo mabaya ya mashambulio ya kijeshi ya nchi za Magharibi dhidi ya Mali. Ripoti ya Umoja wa Mataifa imebainisha kwamba, endapo madola ya Magharibi yataishambulia kijeshi Mali, zaidi ya watu khamsini na tano elfu wa kaskazini mwa nchi hiyo watakuwa wakimbizi. Kufuatia kushuhudiwa hali ya mchafukoge kaskazini mwa Mali, madola ya Magharibi ikiwemo Marekani na Ufaransa yametoa pendekezo la uingiliaji wa kijeshi katika nchi hiyo, ilhali baadhi ya nchi za eneo ikiwemo Algeria zinapinga pendekezo hilo. Umoja wa Mataifa umesema kuwa, katika kipindi cha miezi saba ya ukosefu wa amani katika nchi hiyo kutokana na harakati za waasi, watu wapatao lakini tatu wa kaskazini mwa Mali wamekimbilia katika nchi za Niger na Algeria.

0 comments:

Post a Comment