Sikiliza Live
Sunday, 11 November 2012
Kuanza kazi mitambo ya nyuklia ya Bushehr - Iran
Mkuu wa Taasisi ya Nishati ya Nyuklia wa Jamhuri ya Iran
amesema kuwa, katika kipindi cha miezi michache ijayo, zitafunguliwa
rasmi shughuli za awali za mitambo ya nyuklia huko Bushehr kusini mwa
Iran. Fereydun Abbasi ameongeza kuwa, mitambo ya nyuklia ya Bushehr
itafunguliwa mwezi Januari au Februari mwakani na wataalamu wa Kiirani
baada ya kufanyika majaribio kadhaa ya kitaalamu. Ameongeza kuwa,
shughuli za wakandarasi wa Kirussia zinafikia ukingoni na limebakia
suala la kukabidhiwa rasmi wataalamu wa Kiirani kuiendesha mitambo hiyo.
Abbasi ameongeza kuwa, hivi sasa mitambo ya Bushehr ina uwezo wa
kuzalisha megawati elfu moja za umeme, na kisha kiwango hicho
kitaongezwa kufikia megawati elfu nne hadi sita na hatimaye kuingizwa
kwenye gridi ya taifa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


0 comments:
Post a Comment