Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Sunday, 11 November 2012

Kuna udharura wa kuingilia kijeshi Mali

Rais wa Nigeria amesema kuwa, ni jambo lenye udharura kutumiwa njia ya kijeshi huko kaskazini mwa Mali. Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria amesema mwanzoni mwa kikao cha wakuu wa Kiafrika huko Abuja kuwa uingiliaji wa kijeshi kwa ajili ya kuwafukuzia mbali wapiganaji wa Kiislamu wenye misimamo mikali huko kaskazini mwa Mali na kuzuia taathira zake kuenea katika nchi za Kiafrika ni jambo lenye udharura. Rais wa Nigeria amesema mwanzoni kwa kikao hicho cha dharura cha wakuu wa nchi za Kiafrika huko Abuja kuwa Nigeria itaidhinisha kikamilifu mapendekezo ya Mawaziri wa Mambo ya Nje na Ulinzi wa Kiafrika kwa ajili ya kutuma haraka vikosi vya wanajeshi huko kaskazini mwa Mali ili kurejesha amani na uthabiti katika eneo hilo. Rais wa Nigeria amesisitiza pia kuwa uingiliaji huo wa kijeshi  utategemea azimio la Umoja wa Mataifa.

0 comments:

Post a Comment