Makundi ya upinzani nchini Syria yanayokutana mjini Doha,yamekubaliana
kimsingi kuhusu mpango wa umoja dhidi ya rais Bashar al-Assad.Washiriki
wa mkutano huo wamesema Jumapili(11.11.2012).
"Tumekubaliana kuhusu vipengee viwili juu ya kuundwa kwa muungano wa
kitaifa nchini Syria kwa ajili ya majeshi ya upinzani na mapinduzi.
tutaendelea na majadiliano yetu kuhusu mambo yanayohusika katika
muungano huo leo Jumapili," mmoja wa viongozi wa muungano huo wa
upinzani Suhair Atassi ameliambia shirika la habari la AFP baada ya saa
12 za mazungumzo.
Kiongozi mpya wa SNC George Sabra
"Tulikuwa katika hatua ya kutia saini makubaliano lakini tumeonelea
kutoa muda zaidi ili kutathmini sheria za ndani kwa ombi la baadhi ya
makundi," amesema mjumbe mwingine Riad Seif, ambaye anaripotiwa kuwa
anaonekana na serikali ya Marekani kuwa ana uwezekano wa kuwa mkuu mpya
wa upinzani.Washiriki walitarajiwa kurejea katika mazungumzo leo asubuhi. Mkutano huu unakuja baada ya baraza la taifa la Syria SNC kukabiliwa na mbinyo kutoka kwa mataifa ya Kiarabu na mataifa ya magharibi kukubali mpango wa umoja wa upinzani, huku kukiwa na hali ya kukata tamaa miongoni mwa makundi ya wapiganaji.
Hapo nyuma likiwa linatambulika kama wawakilishi wakuu wa upinzani lakini kadiri ya muda ulivyokwenda lilipoteza hadhi hiyo katika serikali ya Marekani , kutokana na kudhibitiwa na watu ambao wanaishi uhamishoni na hawana uhusiano wa karibu na hali halisi ndani ya nchi, baraza hilo la SNC , lilitakiwa mara mbili kuahirisha mazungumzo juu ya mpango wa kuunda serikali itakayojumuisha makundi mengi ambayo itakuwa inasubiri kuchukua madaraka ndani ya Syria.
Makubaliano hayo yako katika msingi wa harakati zinazochukuliwa na Seif ambazo zina lenga kuundwa kwa serikali ya mpito , ambalo ni baraza la kijeshi litakaloshughulikia makundi ya waasi ndani ya Syria na mahakama ambayo itafanyakazi katika maeneo yanayoshikiliwa na waasi.


0 comments:
Post a Comment