Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Sunday, 11 November 2012

Wapinzani wa Assad wakubali kuugana

Makundi ya upinzani nchini Syria yanayokutana mjini Doha,yamekubaliana kimsingi kuhusu mpango wa umoja dhidi ya rais Bashar al-Assad.Washiriki wa mkutano huo wamesema Jumapili(11.11.2012).
"Tumekubaliana kuhusu vipengee viwili juu ya kuundwa kwa muungano wa kitaifa nchini Syria kwa ajili ya majeshi ya upinzani na mapinduzi. tutaendelea na majadiliano yetu kuhusu mambo yanayohusika katika muungano huo leo Jumapili," mmoja wa viongozi wa muungano huo wa upinzani Suhair Atassi ameliambia shirika la habari la AFP baada ya saa 12 za mazungumzo.
  Kiongozi mpya wa SNC George Sabra
"Tulikuwa katika hatua ya kutia saini makubaliano lakini tumeonelea kutoa muda zaidi ili kutathmini sheria za ndani kwa ombi la baadhi ya makundi," amesema mjumbe mwingine Riad Seif, ambaye anaripotiwa kuwa anaonekana na serikali ya Marekani kuwa ana uwezekano wa kuwa mkuu mpya wa upinzani.


Washiriki walitarajiwa kurejea katika mazungumzo leo asubuhi. Mkutano huu unakuja baada ya baraza la taifa la Syria SNC kukabiliwa na mbinyo kutoka kwa mataifa ya Kiarabu na mataifa ya magharibi kukubali mpango wa umoja wa upinzani, huku kukiwa na hali ya kukata tamaa miongoni mwa makundi ya wapiganaji.
Hapo nyuma likiwa linatambulika kama wawakilishi wakuu wa upinzani lakini kadiri ya muda ulivyokwenda lilipoteza hadhi hiyo katika serikali ya Marekani , kutokana na kudhibitiwa na watu ambao wanaishi uhamishoni na hawana uhusiano wa karibu na hali halisi ndani ya nchi, baraza hilo la SNC , lilitakiwa mara mbili kuahirisha mazungumzo juu ya mpango wa kuunda serikali itakayojumuisha makundi mengi ambayo itakuwa inasubiri kuchukua madaraka ndani ya Syria.
Makubaliano hayo yako katika msingi wa harakati zinazochukuliwa na Seif ambazo zina lenga kuundwa kwa serikali ya mpito , ambalo ni baraza la kijeshi litakaloshughulikia makundi ya waasi ndani ya Syria na mahakama ambayo itafanyakazi katika maeneo yanayoshikiliwa na waasi.

0 comments:

Post a Comment