Rais Francois Hollande wa Ufaransa ameitembela Morocco kwa
minajili ya kuimarisha uhusiano na nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika
koloni lake la zamani, huku wimbi la ufisadi wa mmoja kati ya mawaziri
wa serikali yake likizusha gumzo kubwa nchini. Hollande amelakiwa na
Mfalme Muhammad VI baada ya kuwasili mjini Casablanca ambapo amefuatana
na wafanyabiashara 60 na mawaziri wasiopungua 8 na anatarajiwa leo
kuhutubia Bunge la Morocco.
Safari yake hiyo ya siku mbili nchini Morocco imeathiriwa na sakata la kukwepa kodi linalomkabiliwa waziri wa bajeti wa zamani wa Ufaransa. Jerome Cahuzac amekiri kuwa alikwepa kulipa kodi ya fedha alizozificha kwenye akaunti yake ya nje kwa muda wa miaka 20. Rais wa Ufaransa kabla ya kuelekea Morocco aliahidi kuwa atakabiliana vilivyo na wanasiasa mafisadi nchini kwake.
Safari yake hiyo ya siku mbili nchini Morocco imeathiriwa na sakata la kukwepa kodi linalomkabiliwa waziri wa bajeti wa zamani wa Ufaransa. Jerome Cahuzac amekiri kuwa alikwepa kulipa kodi ya fedha alizozificha kwenye akaunti yake ya nje kwa muda wa miaka 20. Rais wa Ufaransa kabla ya kuelekea Morocco aliahidi kuwa atakabiliana vilivyo na wanasiasa mafisadi nchini kwake.
0 comments:
Post a Comment