Wachezaji Waislamu wa timu ya Soka ya Newcastle United katika Ligi ya
Premier huko England wameonywa kuwa kuvaa jezi zenye nembo ya mfadhili
mpya wa timu hiyo ni ukiukaji wa sheria za Kiislamu.
Newcastle imetangaza mkataba wa Pauni £ Milioni 24 na shirika lenye
utata la kutoa mikopo lijulikanalo kwa jila la Wonga. Sheikh Ibrahim
Mogra Naibu Katibu Mkuu wa Baraza la Waislamu Uingereza amesema kuwa,
shirika la Wonga linawakandamiza sana watu masikini kwa kuwatoza kiasi
kikubwa cha riba kwa mikopo ya muda mfupi. Wachezaji Waislamu katika
timu ya Newcastle ambao ni Demba Ba, Papiss Cisse, Cheick Tiote na Hatem
Ben Arfa wametakiwa watangaze msimamo wao kuhusu suala hili.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


0 comments:
Post a Comment