Sikiliza Live
Sunday, 21 October 2012
Meli ya misaada ya Estelle yashambuliwa na Israel
Katibu Mkuu wa Kamati ya Ubunifu wa Taifa la Palestina amesema kuwa
vikosi vya majini vya Israel vimekiuka wazi sheria za kimataifa kwa
kushambulia meli ya misaada ya kibinadamu ya Estelle katika maji ya
kimataifa. Mustapha Barghuthi ameongeza kuwa, shambulio hilo linaonyesha
pia kushindwa na kugonga ukuta Baraza la Mawaziri la Benjamin Netanyahu
ambalo linaendeleza hatua mbalimbali za jinai. Baraghuthi pia amesema
kuingia meli ya Estelle katika maji ya kimataifa kunaonyesha kufanikiwa
juhudi zake za kuvunja mzingiro wa Gaza na kwamba meli hiyo haijakiuka
sheria yoyote ya kimataifa. Pia amezitaka nchi zote duniani kulaani
hatua hiyo ya uharamia wa baharini na kuifikisha Israel katika vyombo
vya sheria. Juzi vikosi vya majini vya Israel vilishambulia meli ya
misaada ya kibinaadamu iliyotokea Ulaya ambayo ilikuwa imebeba misaada
na wanaharakati mbalimbali wa haki za binadamu kutoka nchi 30 duniani,
na kuizuia kutia nanga katika Ukanda wa Gaza. Meli hiyo imepeleka katika
bandari inayodhibitiwa na Israel ya Ashdod.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment