Serikali ya Libya imetangaza kuwa Khamis Gaddafi mwana mdogo wa
Muammar Gaddafi ameuawa katika mapigano makali yaliyojiri katika mji wa
Bani Walid.
Naibu Waziri Mkuu wa Libya Mustafa Abu Shagur amethibitisha habari za kuuawa Khamis Gaddafi na kusema mwili wake uko katika hospitali ya Misrata kaskazini mashariki mwa Bani Walid.
Khamis ambaye ni mwana wa saba na mdogo zaidi wa dikteta Gaddafi ameuawa baada ya vikosi vya serikali kuuzingira mji wa Bani Walid kwa lengo la kuwatimua wanamgambo watiifu kwa dikteta aliyeuawa Muammar Gaddafi.
Imearifiwa kuwa watu wengine 26 wameuawa katika mapigano hayo huku wengine wengi wakijeruhiwa.
Naibu Waziri Mkuu wa Libya Mustafa Abu Shagur amethibitisha habari za kuuawa Khamis Gaddafi na kusema mwili wake uko katika hospitali ya Misrata kaskazini mashariki mwa Bani Walid.
Khamis ambaye ni mwana wa saba na mdogo zaidi wa dikteta Gaddafi ameuawa baada ya vikosi vya serikali kuuzingira mji wa Bani Walid kwa lengo la kuwatimua wanamgambo watiifu kwa dikteta aliyeuawa Muammar Gaddafi.
Imearifiwa kuwa watu wengine 26 wameuawa katika mapigano hayo huku wengine wengi wakijeruhiwa.
0 comments:
Post a Comment