Sikiliza Live
Saturday, 20 October 2012
Maulamaa wa Russia wapinga marufuku ya hijabu
Baraza la Ulamaa nchini Russia limepinga vikali vitendo vya kibaguzi
vinavyofanywa dhidi ya wanafunzi wanaovaa hijabu ya Kiislamu kwenye
shule za nchi hiyo. Baraza la Ulamaa la Russia ni taasisi kubwa zaidi ya
Kiislamu nchini humo, imeeleza kukerwa na kulaani vitendo vya
unyanyasaji dhidi ya wanafunzi wanaovaa hijabu ya Kiislamu kwenye shule
za eneo la Stavropol nchini humo. Taarifa ya baraza hilo imeeleza kuwa,
Waislamu kwa karne kadhaa sasa wamekuwa wakiishi kwa amani na upendo na
wafuasi wa dini nyingine nchini humo. Taarifa ya baraza hilo imeeleza
kuwa, mwanamke wa Kiislamu anayo haki ya kuvaa hijabu au kitambaa cha
kichwani na kupiga picha itakayotumika kwenye hati ya kusafiria au
kitambulisho cha uraia nchini Russia. Baraza la Ulamaa nchini Russia
limewataka walimu wakuu na walimu wengine kuwaeleza wanafunzi thamani za
kimaadili na kuwasihi wasijitumbukize kwenye vitendo vichafu, na siyo
kuwanyima haki zao za kuvaa hijabu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment