Serikali ya Misri imeutaka Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya
Nyuklia IAEA ukagua mitambo ya silaha za nyuklia ya utawala wa Kizayuni
wa Israel.
Amr Roushdy Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa Misri amesema kuwa, ujumbe wa Cairo kwenye Umoja wa Mataifa umeutaka wakala wa IAEA kukagua mitambo ya silaha za nyuklia ya utawala wa Israel. Roushdy ameongeza kuwa, Mootaz Ahmadein Khalil, Balozi wa Kudumu wa Misri kwenye Umoja wa Mataifa ametoa taarifa hiyo mbele ya kikao cha Baraza Kuu la umoja huo na kuongeza kwamba, utawala ghasibu wa Israel unapuuza maazimio ya Umoja wa Mataifa.
Mootaz Ahmadein Khalil amesema kwamba, utawala ghasibu wa Israel pekee ndio unaozakisha silaha za nyuklia katika eneo la Mashariki ya Kati, jambo ambalo ni hatari na yumkini likazidisha silaha za nyuklia katika eneo hili na hatimaye kukwamisha mpango wa kulifanya eneo hili kutokuwa na silaha za nyuklia.
Amr Roushdy Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa Misri amesema kuwa, ujumbe wa Cairo kwenye Umoja wa Mataifa umeutaka wakala wa IAEA kukagua mitambo ya silaha za nyuklia ya utawala wa Israel. Roushdy ameongeza kuwa, Mootaz Ahmadein Khalil, Balozi wa Kudumu wa Misri kwenye Umoja wa Mataifa ametoa taarifa hiyo mbele ya kikao cha Baraza Kuu la umoja huo na kuongeza kwamba, utawala ghasibu wa Israel unapuuza maazimio ya Umoja wa Mataifa.
Mootaz Ahmadein Khalil amesema kwamba, utawala ghasibu wa Israel pekee ndio unaozakisha silaha za nyuklia katika eneo la Mashariki ya Kati, jambo ambalo ni hatari na yumkini likazidisha silaha za nyuklia katika eneo hili na hatimaye kukwamisha mpango wa kulifanya eneo hili kutokuwa na silaha za nyuklia.


0 comments:
Post a Comment