Kisauji ambaye ni Meya Mstaafu wa Jiji la Tanga, aliwataka wananchi
kutowafumbia macho watendaji wabovu na badala yake watoe taarifa zao
kwa viongozi ili waweze kuchukuliwa hatua.
“Wananchi msisubiri matatizo yakaendeleo kuwa kero, mbona madaraka
sasa yameletwa kwenu huku chini, tatizo liko wapi?...elezeni kwa wakubwa
watu ambao ni kikwazo wawajibishwe” alisema Kisauji.
Aliwataka wananchi kuacha kuwafumbia macho watendaji wabovu kwani
wao ndiyo wahanga na kwamba watu hao pia wanakichafua Chama cha
Mapinduzi kwa kuonekana kimeshindwa kufanyakazi.
Kwa upande mwingine, Kisauji alisema kuwa lengo la serikali ni
kuwawezesha wafanyabiashara wenye mikakati ya kuwekeza kwa kuandaa
mazingira mazuri yakuwafanya watoe huduma bora kwa wananchi.
Mkurugenzi wa Mtandao wa Wanawake wa Inuka unaosimamia chuo hicho,
David Msuya, alieleza kuwa jumla ya wanafunzi 30 wamejiunga tangu
kuanzishwa kwake mapema mwaka huu.
Alitaja kozi 14 zinazotolewa chuoni hapo kuwa ni, utunzaji
kumbukumbu na nyaraka za serikali, hoteli, uhasibu, ujasiliamali, ufundi
cherahani, uongozi, utawala na ualimu wa chekechea.
Kozi nyingine ni uandishi wa habari, sheria za michezo, uongozi wa
watalii, mawasiliano kwa umma, kozi za bandari, ukatibu muhtasi na
ukusanyaji wa mapato.
0 comments:
Post a Comment