03 Shaaban,1434
Hijiriyah/ June12 ,2013 Miyladiyah
Katika hali ambayo, Ufaransa bado inashindwa kutangaza ushindi dhidi ya
waasi huko nchini Mali, vyombo vya habari vimeripoti kuanza harakati
mpya za uasi katika nchi mbili za Chad na Niger. Ripoti zaidi zinaeleza
kuwa, kuna uwezekano mkubwa wanamgambo wa Mali waliokimbilia huko kusini
mwa Libya baada ya mashambulizi ya askari wa Ufaransa na Mali dhidi ya
maeneo yao ya kaskazini mwa Mali, nao wakaanzisha mashambulizi mapya
dhidi ya nchi za Chad na Niger na kwamba, viongozi wa nchi hizo hawana
tena utulivu wa moyo kama hapo kabla. Mwanadiplomasia mmoja wa Niger
amenukuliwa akisema kuwa, hadi hivi sasa hali ya mambo haitabiriki na
kwamba, nchi hizo mbili zinaishi kwa wasiwasi mkubwa huku zikiweka
mipango madhubuti ya kuimarisha ulinzi na usalama. Kwa upande wake,
Mathieu Pellerin mtafiti katika Shirika la Mahusiano la Kimataifa la
nchini Ufaransa amethibitisha kuwepo makundi ya wanamgambo huko kusini
mwa Libya na kusisitiza kuwa, wanamgambo hao wamejizatiti kwa silaha
nzito tangu kipindi cha utawala wa Kanal Muammar Gaddafi sambamba na
kuanzisha kambi za mafunzo ya kijeshi katika eneo hilo.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment