Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 15 June 2013

SHEIKH PONDA NI JEMBE - LWAKATARE

                            

 

Mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa CHADEMA, Winfred Lwakatare... alisema "Sheikh Ponda ni Jembe".Akiwa na maana Mtu Jasiri.
Alizungumza hayo baada ya kuachiwa jumanne, Lwakatare ambako baada ya kuongea na wafuasi kadhaa wa CHADEMA alikutana na baadhi ya viongozi na kudokeza machache aliyokutana nayo jela.
"Nimekaa jela siku 92 tangu March 11 hadi June 22, katika selo nilowekwa nilikuwa na Sheikh Ponda.
Akaongeza, ninachoweza kusema ni kuwa Sheikh Ponda ni mtu mwenye upendo na kumcha sana Mungu, lakini zaidi ni msimamo wa kutetea mali za waislamu, ninachofurahishwa ni kuwa na mtu mwenye msimamo.
Lwakatare alisema yaani hata ukizungumza nae unaona mtu huyo anazungumza mambo yenye logic (maana). Amejitokeza kutaka watu wapate mali yao lakini ameonekana kama mchochezi. Kama hujui anachodai unaweza kumuona mbaya, lakini hapana

Chanzo: Gazeti la Kisiwa
Title: Lwakatare asimulia alivyoishi na Ponda gerezani.

0 comments:

Post a Comment