Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 27 June 2013

‘Migongano ya Waislamu inafaidisha Israel, Marekani’





Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Ahmad Vahidi ameonya kuwa Marekani na Utawala haramu wa Israel ndio zinazonufaika na migongano ya kimadhehebu miongoni mwa Waislamu.
Vahidi amelaani mauaji ya hivi karibuni ya Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Misri ambao waliuawa na Mawahabi wanaowakufurisha Waislamu. Vahidi amesema Mawahabi wanaowaua Mashia wanafanya hivyo kwa uchochezi wa Marekani na Israel na kuongeza kuwa, wale wote wanaojali maslahi ya Umma wa Kiislamu wamelaani kitendo hicho cha kinyama. Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema Mashia na Masuni ni ‘mbawa mbili za Uislamu. Ametoa wito kwa Waislamu wanaofuata madhehebu ya Shia na Suni kuungana na kutowaruhusu maadui kuwagawa.
Aghalabu ya wanazuoni wa Kiislamu akiwemo Mkuu wa Chuo Kikuu cha Al Azhar wamelaani vikali ukatili huo wa makundi ya wakufurishaji. Inafaa kuashiria hapa kuwa Mawahabi wakufurishaji wanaamini kuwa tafsiri yao ya Uislamu ndio sahihi na kwamba eti Waislamu wengine wote ni makafiri. Kwa karne nyingi sasa Waislamu wa madhehebu zote wamekuwa wakiishi kwa amani na maelewano nchini Misri na kote duniani.

0 comments:

Post a Comment