03 Shaaban,1434
Hijiriyah/ June12 ,2013 Miyladiyah
Jengo la Waislamu la Somali Bravanese Welfare Association lililoteketezwa moto London wiki iliyopita.
Imeelezwa kuwa vitendo na miamala mibaya dhidi ya jamii ya Waislamu
nchini Uingereza vimeongezeka maradufu katika siku za hivi karibuni
baada ya kuuawa askari mmoja wa Uingereza, huko kusini mashariki mwa
London. Hayo yameelezwa na Kamanda wa Polisi mjini London Simon
Latchford na kuongeza kuwa, vitendo vya kibaguzi dhidi ya Waislamu,
vimeongezeka kwa asilimia nane. Amesema vitendo hivyo vimeongezeka
katika hali ambayo awali vilikuwa sawa na asilimia moja tu. Aidha afisa
huyo wa polisi mjini London amekiri kuwa, baadhi ya vitendo kama hivyo
haviripotiwi kwa polisi na wala kwa vyombo vya habari nchini humo. Hii
ni katika hali ambayo, baada ya kuchomwa moto shule moja ya Waislamu
huko kusini mwa mji mkuu wa Uingereza, London, polisi ilitangaza
kuzidisha doria katika maeneo tofauti ya mji huo ili kuilinda jamii
Waislamu mjini humo. Mauaji ya askari Lee Rigby yaliyotokea katika eneo
la Woolwich, kusini mashariki mwa London, yanatajwa kuwa chanzo cha
kuongezeka ubaguzi dhidi ya jamii ya Waislamu nchini Uingereza.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment