Jumuiya ya Nchi za Kiarabu ' Arab League' umeamua kuanzisha Mfuko wa
Maendeleo na Uwekezaji nchini Komoro utakaokuwa na thamani ya dola
milioni mia tano. Sheikh Ahmad bin Muhammad Aal Thani Naibu Waziri wa
Mambo ya Nchi za Nje wa Qatar anayehusika na mashirikiano ya kimataifa
na ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya maendeleo na uwekezaji wa
jumuiya hiyo nchini Komoro amesema kuwa, mfuko huo umeanzishwa kwa lengo
la kuunga mkono na kutekelezwa miradi ya kimaendeleo na ya uwekezaji
visiwani humo. Amesema kuwa, lengo kuu la kuanzishwa mfuko huo ni
kuinasua nchi hiyo na lindi la umasikini. Inafaa kuashiria hapa kuwa,
Visiwa vya Komoro licha ya kuwa ni mwanachama wa Jumuiya ya Nchi za
Kiarabu 'Arab League' ni mwanachama pia wa Jumuiya ya Ushirikiano wa
Kiislamu OIC.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment