Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 13 June 2013

Kampeni za uchaguzi wa rais wa Iran zamalizika rasmi



 Wagombea wa uchaguzi wa rais nchini Iran wamemaliza rasmi kampeni zao leo saa mbili asubuhi. Akihutubia katika mji wa Birjand kusini mwa nchi, Ali Akbar Velayati alisema, baraza la mawaziri linapaswa kuwa la wataalamu na kwamba wanapaswa kusaidia vijana wenye vipaji kuendeleza nchi. Mgombea Saed Jalili amefunga kampeni zake za uchaguzi huko mkoani Golestan ambapo amewaambia wafuasi wake kuwa, Iran ina uwezo wa kutatua matatizo yake ya ndani kama vile ughali wa maisha na ukosefu wa ajira, kama ilivyoweza kusimama kidete dhidi ya maadui. Mohsen Rezai ameeleza katika mahojiano na waandidhi habari kwamba, sera zake yeye ni kutoonyesha msimamo mkali iwapo Wamagharibi watataka kulegeza misimamo yao na kwamba ni bora Wamagharibi waondoe vikwazo ili kuimarisha uhusiano wa kibiashara wa pande mbili na kuimarisha uchumi wao. Naye Mohammad Gharazi amesema, kila mkoa unapaswa kuendesha mambo yake wenyewe na baadaye kuripoti kwa serikali kuu. Mgombea Muhammad Qalibaf alihitimisha kampeni zake mjini Isfahani ambako alitoa wito kwa wananchi wajitokeze kwa wingi kupiga kura na kuahidi kuleta maendeleo makubwa ya kiuchumi iwapo atachaguliwa. Hii ni katika hali ambayo Hassan Rohani ameahidi kuimarisha uhusiano na nchi za dunia, akisema kwamba serikali yake itayapa kipaumbele matatizo ya uchumi. Uchaguzi wa rais wa Iran utafanyika kesho Ijumaa, Juni 14.

0 comments:

Post a Comment