Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 18 May 2013

Wanafunzi 7,338 hawajaripoti sekondari

 
JUMLA ya wanafunzi 7,338 hawakujiunga katika shule mbalimbali za sekondari za kata wilayani Karagwe, Kagera katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2012.
Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Darry Rwegasira alibainisha hayo jana alipokuwa akiwatuhumu madiwani wa halmashauri hiyo kwenye Ukumbi wa Rafiki wa Angaza uliopo wilayani hapa.
Alisema wanafunzi hao hawakujiunga na elimu ya sekondari pamoja na kufaulu mtihani wa taifa katika kipindi hicho.
“Tuwaandalie watoto wetu urithi wa elimu kuliko tabia zilizopo za kuchangia harusi na kuwasahau watoto ambao ndio watakaolikomboa taifa hili kwa nyanja zote,” alisema Rwegasira.
Alibainisha katika mwaka 2010 wanafunzi waliochaguliwa walikuwa 5,150. Kati ya hao 1,177 hawakuripoti shuleni, mwaka 2011 wanafunzi 5,107 walichaguliwa na 2,155 hawakuripoti shule na katika mwaka 2012 kati ya 8,871 wanafunzi 4,006 hawakuripoti shuleni.
Hata hivyo, alisema shule nyingi za sekondari katika wilaya hiyo hazina miundombinu iliyodumu kutokana na baadhi ya wazazi kutokuwa na mwamko wa kuchangia maendeleo ya shule na kuongeza kuwa kata ambazo hazina sekondari za kata zimekuwa na tatizo katika kuchangia maendeleo ya shule za kata zilizo jirani.

0 comments:

Post a Comment