23Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ May 03,2013 Miyladiyah
Waasi wa kundi linalopigania kujitenga eneo la Cabinda nchini Angola
FLEC wamesema wako tayari kuweka silaha chini na kuzungumza na serikali
ya nchi hiyo. Waasi hao wamesema mazungumzo yoyote kati yao na serikali
sharti yatilie maanani kilio cha miaka mingi cha wakaazi wa eneo hilo.
FLEC imekuwa ikipigania kujitenga eneo hilo lililoko kaskazini mwa mji
mkuu wa Angola, Luanda kwa miongo kadhaa sasa. Cabinda ni eneo lenye
utajiri mkubwa wa mafuta lakini wakaazi wake wanaishi katika hali mbaya
ya umasikini. Kundi la FLEC lilitangaza kusitisha vita mwaka 2006 dhidi
ya serikali ya Angola lakini hadi sasa limekuwa likifanya mashambulizi
ya kuvizia. Itakumbukwa kuwa, mwaka 2010 kundi hilo lilishambulia timu
ya taifa ya Togo ilipokuwa ikielekea Angola kushiriki mashindano ya soka
ya mataifa bingwa barani Afrika.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment