Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 21 May 2013

UK yataka mgogoro wa Syria utatuliwe kwa amani



 Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Uingereza ametaka mgogoro wa Syria utatuliwe kwa njia za kisiasa. Akizungumza mbele ya bunge la nchi hiyo, William Hague ameongeza kuwa, mgogoro wa Syria hauwezi kutatuliwa kwa njia za kijeshi na hivyo ameitaka serikali ya Damascus na makundi ya waasi nchini humo kufanya mazungumzo ili kukomesha mgogoro nchini humo. Hata hivyo, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uingereza amesisitiza azma ya London ya kuendeleza  uungaji mkono wake  kwa makundi ya kigaidi nchini Syria na kubainisha kuwa, katika kikao kijacho cha Umoja wa Ulaya, London itatoa pendekezo la kurekebishwa na kulegezwa vikwazo vya silaha vilivyowekwa na umoja huo dhidi ya makundi ya kigaidi nchini Syria. Matamshi ya Hague yanatolewa katika hali ambayo, Marekani, Uingereza, Ufaransa na hali kadhalika Saudi Arabia, Qatar na Uturuki ziko mstari wa mbele katika kushadidisha mgogoro wa Syria kwa kuyapa misaada ya silaha na fedha makundi ya kigaidi nchini humo.

0 comments:

Post a Comment