Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 28 May 2013

Rais wa Sudan: Hatutafanya mazungumzo na waasi




Rais Omar Hassan al Bashir wa Sudan amesema kuwa, Khartoum haitafanya mazungumzo na waasi wa Muungano wa Harakati ya Kimapinduzi ya nchini humo.  Akizungumza na vyombo vya habari makao makuu ya jeshi mara baada ya majeshi ya Sudan kuukomboa mji muhimu katika jimbo la Kordofan Kusini, Rais al Bashir amesisitiza kama ninavyonukuu:"Kamwe hatutafanya mazungumzo na vibaraka na magaidi ambao wenyewe wanajiita harakati ya kimapinduzi." Harakati ya Kimapinduzi ni muungano wa makundi matatu yaliyoko Darfur na yamekuwa yakipambana na serikali tokea mwaka 2003. Makundi hayo matatu ni Harakati ya Uadilifu na Usawa, Harakati ya Ukombozi wa Sudan tawi la Mini Minawi na tawi la AbdulWahid Nour na kwa upande mwingine, Harakati ya Wananchi iliyoko kaskazini mwa Sudan nayo imekuwa ikipambana na serikali katika mikoa ya Kordofan na Blue Nile tokea mwaka 2011.

0 comments:

Post a Comment