Rais Hifikepunye Lucas Pohamba wa Namibia
Rais Hifikepunye Lucas Pohamba wa Namibia ametangaza hali ya hatari
iliyosababishwa na ukame mkubwa unaoikabili nchi hiyo. Rais Pohamba
ameongeza kuwa, ukame mkubwa unaoikabili nchi hiyo umesababishwa na
kiwango kidogo cha mvua, na bila shaka utaleta taathira mbaya kwa maisha
ya wananchi wa nchi hiyo. Rais Pohamba amesisitiza kuwa, ukame wa mwaka
huu utaliathiri taifa lote la Namibia na kuna uwezekano mkubwa kiwango
cha mavuno ya nafaka kushuka na kufikia hata chini ya asilimia 48 katika
badhi ya maeneo ya nchi hiyo.
0 comments:
Post a Comment