Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Wednesday 22 May 2013

RAIS KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA IRINGA-DODOMA

 Rais Jakaya  kikwete  wa nne  kushoto akiwa na  viongozi mbali mbali akiwemo  waziri  wa ujenzi Dkt John Magufuli wa wa sita  na waziri  wa nchi ofisi ya  waziri mkuu  sera na uratibu wa bunge na mbunge wa jimbo la Isimani Bw. Wiliam Lukuvi nyuma viongozi wa  mahakama na viongozi  wa serikali
  Picha ya pamoja na  watumishi  wa TANROADS mkoa  wa Iringa na Rais Jakaya  Kikwete

 Rais Kikwete  akiwa katika picha ya pamoja na  v iongozi wa dini mkoa  wa Iringa waliosimama nyuma

Rais  Kikwete akiangana na wananchi  waliofika kushuhudia zoezi la uwekaji jiwe la Msingi barabara  ya lami kati ya Iringa - Dodoma
 Rais  Kikwete akiwa katika  picha ya pamoja na madiwani Iringa 


RAIS Jakaya  Kikwete  ameweka  jiwe la msingi katika  ujenzi  wa barabara  ya  Iringa - Dodoma na  kuwaonya  watu  wanaoendelea  kuhujumu miundo mbinu kwa kuiba  alama  za barabarani .
Rais Kikwete  alisema  kuwa mbali ya  serikali  kujipanga katika kuhakikisha kuwa nchi nzima inaunganishwa na mtandao  wa barabara  za lami  ila bado baadhi ya  watu  wamekuwa  wakifanya hujuma  katika barabara bila kuangalia fedha ambazo  serikali imetumia katika ujenzi  wa barabara  hiyo na kuwataka  wananchi  kuwa  walinzi  wa barabara  hizo .
Akizungumza na  wananchi  wa jimbo la Isimani katika eneo la Migoli - Mtera  wakati  wa uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi  wa barabara  ya Iringa - Dodoma leo ,Rais Kikwete  alisema  kuwa ili  kuendelea  kutunza barabara  hizo ni vema  wanaohujumu miundo mbinu  kufichuliwa na kuchukuliwa hatua kali.
Hata  hivyo  alisema mbali ya  serikali kuendelea  na uboreshaji  wa miundo mbinu hapa  nchini bado anawataka  watanzania  kutambua jitihada  hizo .
Alisema kuwa  sasa  watanzania  wanaweza kusafiri hadi Kenya na Uganda  kwa barabara ya lami na kuwa bado jitihada  zitaendelea daima.
 Rais   Kikwete  alisema  kuwa  mbali ya  serikali  kujipanga kwa  ujenzi  wa barabara bado lengo la  serikali ni  kuhakikisha nchi  nzima inaunganishwa kwa mtandao  wa barabara  ya lami na kuwa kazi hiyo tayari  imeanza.
Alisema  kuwa serikali  yake  toka  imeingia madarakani  imeendelea  kuongeza  fedha  katika mfuko  wa barabara  na kuwa lengo ni kuendelea  kuongeza  zaidi fedha katika mfuko  huo ili  kuwezesha  ujenzi  wa barabara nchini kuweza  kukamilika 
 Rais  Kikwete  pia amewapongeza  viongozi wa TANROADS kwa kazi nzuri  wanayoendelea  kuifanya na kwa  mbali ya kupongezwa bado hawapaswi kulewa  sifa na badala  yake  kuendeleza  jitihada za  kusimamia  kazi  hiyo kwani upo usemi unao sema kuwa mgema akisifiwa pombe huweka maji .
Pia  Rais Kikwete alimpompongeza  waziri wa fedha Dkt Wiliam Mgimwa kwa kuendelea  kuidhinisha  fedha kwa ajili ya miradi ya barabara hapa nchini na kuwa  bila  wizara  hiyo  kutenga bajeti  kazi hiyo ingeendelea  kuwa ngumu.
Akizungumzia kuhusu amani na utulivu nchini Rais Kikwete  alisema  wapo  baadhi ya  watu usiku na mchana  wamekuwa  wakipanga mipango mibaya ya  kuvuruga amani ya nchi  hii na hivyo noi vema  watanzania kuwaepuka  watu wenye nia ya kuchafua nchi hii kwa kuchochea  vurugu.
Alisema  iwapo  watanzania  watakataa kuwasikiliza watu hao wala kushirikiana nao  kamwe Tanzania haitaingia katika machafuko yanayopangwa na watu hao  wasio penda mema.
Kwa upande  wake mbunge wa  jimbo la Isimani wilayani  Iringa mkoani Iringa  Bw. Wiliam Lukuvi alimpongeza  Rais Jakaya  Kikwete  kwa  kuwawezesha  wakazi  wa tarafa  ya Isimani kuweza  kuanza  kushuhudia mapinduzi makubwa ya  kimaendeleo kupitia mradi mkubwa  wa barabara  ya  kiwango  cha lami kutoka Iringa - Dodoma  inayopita katika   tarafa  hiyo .
Lukuvi  ambae ni  waziri  wa nchi  ofisi  ya  waziri  mkuu (sera na uratibu  wa  bunge) alisema  kuwa  barabara  hiyo ambayo ni ukombozi mkubwa kwa nchi  za  kusini mwa  Tanzania  ilikuwemo katika mkakati  wa kujengwa kwa kiwango  cha lami kwa kitambo  kirefu na  kila awamu  wananchi  walikuwa  wakiulizana  juu ya kuanza  kwa mradi huo.
Hata  hivyo  alisema  baada ya awamu  hii ya nne  chini ya  Rais Kikwete  wananchi hao  wameweza kushuhudia  majibu ya maswali yao  kwa  kuanza  kwa ujenzi huo ambao  kila mmoja anatambua  kama ni ukombozi katika  sekta ya maendeleo.
Waziri  Lukuvi alitoa  pongezi  hizo kwa Rais Kikwete   wakati akiwasalimia  wananchi  wa  jimbo  la Isimani ambao  walishiriki hafla  fupi ya Rais Kikwete  kuweka jiwe 
Akitoa  taarifa  ya ujenzi  wa barabara  hiyo waziri wa ujenzi Dkt John Magufuli alisema  kuwa  wizara yake haitasita kuwachukulia hatua  makandarasi ambao  watashindwa kutekeleza mikataba yao kama ilivyo elekezwa.
Waziri Magufuli alisema  kuwa  wizara  yake chini ya Rais Kikwete  itaendelea  kusimamia  ujenzi  wa barabara na kujenga kwa kiwango cha lami na  kuwa  wale  wanaopinga  jitihada hizo  waendelee kusubiri kuandamana katika barabara  zilizojengwa na serikali ya CCM.
Katika hatua  nyingine Dkt Magufuli alimpongeza mbunge wa jimbo la Isiman ,Lukuvi kuwa ni mbunge na  waziri mchapa kazi na kuwa iwapo angekuwa jimboni kwake na kutangaza kugombea ubunge basi angemwachia jimbo ili agombee.
Waziri Magufuli alisema kuwa ujenzi wa barabara  hiyo ya Iringa -Dodoma yenye urefu wa Km 260  itajengwa kwa zaidi ya bilioni 232 fedha kutoka benki ya maendeleo Afrika (ADB) na serikali ya Japani pamoja na serikali ya Tanzania.
Wakati  huo  huo  wafanyakazi  na vibarua  wanaofanya kazi katika kampuni  hiyo ya kichina  inayotengeneza  barabara  ya eneo la Migoli katika barabara hiyo ya Iringa - Dodoma nusuru  wavurugu siku baada ya kupaza  sauti mbele ya  Rais wakilalamikia   fedha kiduchu  wanazo  pata kwa siku kwa kufanya kazi katika kampuni hiyo.
Vibarua  hao  na  wafanyakazi  walisikika  wakipaza sauti  wakati Rais Kikwete akiaga kwa ajili ya kuelekea katika chakula  cha mchana kuwa wanapunjwa  sana mishahara na kuomba kusaidia kupiganiwa  ili kulipwa kima cha chini cha mishahara ya  serikali.
"Mheshimiwa  Rais una ondoka  ila sisi  wafanyakazi tunaomba kusikilizwa kilio chetu ....hawa  wachina  wanatufanyisha kazi kwa ujira mdogo sana mheshimiwa tunaomba kusaidiwa ....walipasa  sauti wafanyakazi na vibarua hao ambao  walikuwa wamesimama  juu ya mashine  zao za kazi"
Hata  hivyo Rais Kikwete hakuweza  kujibu  chochote  juu ya madai hayo kutokana na eneo  hilo kutawaliwa na kelele nyingi za burudani na hivyo kushindwa  kusikia zaidi ya mkuu  wa mkoa wa Iringa Dkt Christine Ishengoma  kuwasikia na  kuwajibu kwa  sauti ya chini kuwa ila si mnapata chakula?

0 comments:

Post a Comment