Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 2 May 2013

Kagasheki jiuzulu

Kambi rasmi ya upinzani bungeni, imesema ni muda mwafaka kwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki kujiuzulu kutokana na ama kwa kujua, au kutojua kuongoza njama za makusudi kutaka kumpatia mwekezaji wa Kampuni ya Otterlo Business Corporation (OBC) katika ardhi ya Loliondo.
Akiwasilisha maoni ya kambi hiyo kuhusu Makadirio ya Matumizi kwa mwaka 2013/14 ya Wizara ya Maliasili na Utalii juzi, Msemaji Mkuu wa kambi hiyo, Mchungaji Peter Msigwa alisema ardhi hiyo wanataka kuitoa kinyume cha sheria.“Huu ni wakati mwafaka kwa Waziri Kagasheki kuwajibika kwa kujiuzulu kwa hiari yake, au kama atashindwa kufanya hivyo, kuwajibishwa kwa kufukuzwa kazi kwa kusababisha mgogoro wa sasa maeneo ya Loliondo na Sale,” alisema.
Alitaka kujua kama ni kweli kitendo cha hivi karibuni cha Waziri Kagasheki kutoa amri ya wananchi wa Loliondo na Sale kunyang’anywa maeneo yao mengine na kukabidhiwa kwa Kampuni ya OBC, kilitokana na maagizo au maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
Mchungaji Msigwa alisema kutokana na Kamati iliyoundwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuchunguza mgogoro huo na kuongozwa na Naibu Katibu Mkuu CCM bara, Mwigulu Nchemba inaonyesha uamuzi huo ulikuwa uamuzi wake.
Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi aliilaumu kambi hiyo akisema inatoa kauli ya uongo ili hali ikijua ukweli kuhusu tuhuma dhidi ya Kinana.
Nchimbi alisema mmiliki wa meli ile anaitwa Bus Herman Ledley na walituhumiwa na kupelekwa mahakamani kwa kosa hilo kuwa ni pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya Team Fright (T) Ltd, Ladius Tesha, Gabriel Chambo wa Kampuni ya Import and Export Ltd, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Kigoma MN Enterprises Ltd, Shaaban Yasin Abdullah, mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bandari ya Dar es Salaam, Ericleo Morani, mfanyakazi wa Kampuni ya Kigoma MN Enterprises, Issa Ahmed Rwino na Mawakala wa Kampuni ya T Fright (T) Ltd, Nelbert Kiwale na Abubakar Omar Hassan.

0 comments:

Post a Comment