Kambi rasmi ya upinzani bungeni, imesema ni muda mwafaka kwa
Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki kujiuzulu
kutokana na ama kwa kujua, au kutojua kuongoza njama za makusudi kutaka
kumpatia mwekezaji wa Kampuni ya Otterlo Business Corporation (OBC)
katika ardhi ya Loliondo.
Akiwasilisha maoni ya kambi hiyo kuhusu Makadirio
ya Matumizi kwa mwaka 2013/14 ya Wizara ya Maliasili na Utalii juzi,
Msemaji Mkuu wa kambi hiyo, Mchungaji Peter Msigwa alisema ardhi hiyo
wanataka kuitoa kinyume cha sheria.“Huu ni wakati mwafaka kwa Waziri
Kagasheki kuwajibika kwa kujiuzulu kwa hiari yake, au kama atashindwa
kufanya hivyo, kuwajibishwa kwa kufukuzwa kazi kwa kusababisha mgogoro
wa sasa maeneo ya Loliondo na Sale,” alisema.
Alitaka kujua kama ni kweli kitendo cha hivi
karibuni cha Waziri Kagasheki kutoa amri ya wananchi wa Loliondo na Sale
kunyang’anywa maeneo yao mengine na kukabidhiwa kwa Kampuni ya OBC,
kilitokana na maagizo au maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
Mchungaji Msigwa alisema kutokana na Kamati
iliyoundwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuchunguza mgogoro
huo na kuongozwa na Naibu Katibu Mkuu CCM bara, Mwigulu Nchemba
inaonyesha uamuzi huo ulikuwa uamuzi wake.
Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa
Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi aliilaumu kambi hiyo akisema inatoa
kauli ya uongo ili hali ikijua ukweli kuhusu tuhuma dhidi ya Kinana.
Nchimbi alisema mmiliki wa meli ile anaitwa Bus
Herman Ledley na walituhumiwa na kupelekwa mahakamani kwa kosa hilo kuwa
ni pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya Team Fright (T) Ltd, Ladius
Tesha, Gabriel Chambo wa Kampuni ya Import and Export Ltd, Mkurugenzi
Mkuu wa Kampuni ya Kigoma MN Enterprises Ltd, Shaaban Yasin Abdullah,
mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bandari ya Dar es
Salaam, Ericleo Morani, mfanyakazi wa Kampuni ya Kigoma MN Enterprises,
Issa Ahmed Rwino na Mawakala wa Kampuni ya T Fright (T) Ltd, Nelbert
Kiwale na Abubakar Omar Hassan.
0 comments:
Post a Comment