Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 25 May 2013

Niger wamkomboa mwanajeshi mikononi mwa waasi

                                            15 Rajab,1434 Hijiriyah/ May 25,2013 Miyladiyah
 Karidjo Mahamadou Waziri wa Ulinzi wa Niger amesema kuwa, vikosi vya jeshi la nchi hiyo vikishirikiana na vya Ufaransa vimefanya oparesheni kubwa katika mji wa Agadez na kufanikiwa kumuokoa mwanajeshi wa nchi hiyo aliyekuwa akishikiliwa mateka na waasi. Karidjo Mahamadou amesema kuwa, kwenye oparesheni hiyo wateka nyara wawili waliuawa wakati wa kufyatuliana risasi na wanajeshi wa Niger wakishirikiana na wa Ufaransa. Hii ni katika hali ambayo, kabla ya hapo, Waziri wa Ulinzi wa Niger alikuwa amekadhibisha taarifa za kutekwa nyara mwanajeshi wa Niger na kundi la watu wanaobeba silaha nchini humo. Mara baada ya kutokea shambulio la waasi huko kaskazini mwa Niger, Rais Francois Hollande wa Ufaransa alitangaza kuendelea kubaki majeshi ya nchi hiyo barani Afrika kwa kisingizio cha kupambana na makundi ya kigaidi na kuzisaidia nchi za Kiafrika.

0 comments:

Post a Comment