15 Rajab,1434
Hijiriyah/ May 25,2013 Miyladiyah
Karidjo Mahamadou Waziri wa Ulinzi wa Niger amesema kuwa, vikosi vya
jeshi la nchi hiyo vikishirikiana na vya Ufaransa vimefanya oparesheni
kubwa katika mji wa Agadez na kufanikiwa kumuokoa mwanajeshi wa nchi
hiyo aliyekuwa akishikiliwa mateka na waasi. Karidjo Mahamadou amesema
kuwa, kwenye oparesheni hiyo wateka nyara wawili waliuawa wakati wa
kufyatuliana risasi na wanajeshi wa Niger wakishirikiana na wa Ufaransa.
Hii ni katika hali ambayo, kabla ya hapo, Waziri wa Ulinzi wa Niger
alikuwa amekadhibisha taarifa za kutekwa nyara mwanajeshi wa Niger na
kundi la watu wanaobeba silaha nchini humo. Mara baada ya kutokea
shambulio la waasi huko kaskazini mwa Niger, Rais Francois Hollande wa
Ufaransa alitangaza kuendelea kubaki majeshi ya nchi hiyo barani Afrika
kwa kisingizio cha kupambana na makundi ya kigaidi na kuzisaidia nchi za
Kiafrika.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment