Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 30 May 2013

Matokeo kidato cha nne yazidi kuibua mapya

                                 20Rajab,1434 Hijiriyah/ May 30,2013 Miyladiyah
  Matokeo ya kidato cha nne yanayotarajiwa kutangazwa leo, yamezidi kuzua mapya baada ya Baraza la Mitihani nchini (Necta) kulazimika kutumia kanuni iliyofanya ufaulu upande kwa asilimia tisa kutoka 34 wa awali, lengo likiwa ni kuepusha watahiniwa waliokuwa wamefaulu mwanzo kufeli.
Kanuni iliyokuwa imetumika mwanzo, ilifanya matokeo hayo yapande kwa asilimia kati ya 20 na 23, kiwango ambacho Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete aliwaeleza wabunge wa chama chake Mei 19, mwaka huu mjini Dodoma.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kutoka ndani ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, wiki iliyopita maofisa wa wizara na taasisi zake wakiongozwa na Waziri Dk Shukuru Kawambwa, walijadili matokeo hayo.
 “Wakati yakijadili, ufaulu bado ulikuwa kulekule kwenye zaidi ya asilimia 54, kutokana na kanuni hiyo wanafunzi kama 2,500 waliokuwa wamefaulu kwa madaraja ya juu walikuwa washuke,” kilisema.
Kutokana na hali hiyo, kwa sasa ufaulu ni asilimia 43 jambo linalofanya matokeo hayo yawe chini ikilinganishwa na mwaka 2011.
Chanzo chetu kilieleza kuwa, katika kikao hicho, kulikuwa na mvutano kuhusu kanuni ipi itumike ili kuwaokoa wanafunzi hao alama zao zisishuke.
Baada ya kumalizika kwa kikao hicho, Necta ilienda tena kuyafanyia kazi matokeo hayo ambapo sasa ufaulu umeshuka kwa asilimia zaidi ya 20 hadi kufikia  asilimia tisa.
“Kwa sasa hakuna mtu ambaye matokeo yake yameshuka, ila bwana kazi ipo siyo kama ambavyo watu wanaona kuna vurugu kweli,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Ukijaribu kuangalia, Necta wanasimamia kanuni, lakini wakati mwingine inabidi mtu uangalie hali ilivyo, kwa sasa watu wanaangalia zaidi mwitikio wa wananchi utakavyokuwa haya matokeo yakitangazwa badala ya kuangalia vitu vya msingi,” kilisema chanzo hicho.

0 comments:

Post a Comment