Waziri Mkuu wa Iraq Nouri al Maliki amesema kuwa, chama cha Baathi
kilichong'olewa madarakani, ndicho kinachopanga mashambulizi ya kigaidi
nchini humo. Al Maliki ameyasema hayo leo katika kikao na waandishi wa
habari mjini Baghdad, Iraq. Akiashiria kuendelea kwa mashambulizi na
miripuko nchini Iraq amesema, chama hicho cha Baathi kilichokuwa
kikiongozwa na Saddam ndicho kinachopanga mashambulizi hayo na kwamba,
hatua hiyo inaonyesha kuwepo kwa chuki za kikaumu nchini. Amesisitiza
kuwa, viongozi wa chama hicho waliokuwa wakiwafukia watu wakiwa hai
ndani ya kaburi moja, leo hii wafuasi wao wanaratibu na kutekeleza
mashambulio ya mabomu katika maeneo ya watu wengi kama vile masokoni,
misikitini na barabarani na kuwaua raia wengi wasio na hatia. Aidha
waziri mkuu huyo wa Iraq amekosoa hatua ya baadhi ya vyama vya siasa
kuunga mkono chama cha Baathi kilichofutwa nchini humo. Hii ni katika
hali ambayo, mapema leo watu 16 wameuawa na wengine 34 kujeruhiwa katika
miripuko ya mabomu, iliyotokea katika maeneo mawili ya Sadr na Kamaliya
katika viunga vya mji mkuu wa Iraq, Baghdad. Aidha jana watu wengine 35
waliuawa na wengine 134 kujeruhiwa katika miripuko ya mabomu iliyotokea
katika maeneo tofauti nchini humo.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment