Askari wa Algeria kwa kushirikiana na kikosi maalumu cha kulinda mpaka
wa nchi hiyo, wamepambana na magaidi waliokuwa wanakusudia kuvuka mpaka
wa Tunisia kuingia nchini humo. Kiongozi mmoja wa usalama wa Algeria
amesema kuwa, mapigano hayo yalijiri usiku wa jana katika eneo la Buque
Fella lililoko kusini mwa mkoa wa al-Wadi kilometa 600 kusini mashariki
mwa Algeria, kati ya magaidi hao na askari jeshi kwa kushirikiana na
kikosi maalumu cha kulinda mpaka nchini humo. Afisa huyo ambaye
hakutaka jina lake litajwe kwa kuwa yeye siye msemaji wa jeshi, amesema
kuwa, magaidi hayo yalikuwa yanakusudia kupenya mpaka na kuingia eneo
la jangwani nchini Algeria. Katika operesheni hiyo, gaidi mmoja ameuawa
na wengine wawili wametiwa mbaroni. Afisa huyo amesema kuwa, katika
oparesheni hiyo, silaha kadhaa na zana nyingine za magaidi hao kikiwemo
chombo kimoja cha mawasiliano kilichotengezwa Marekani zimedhibitiwa na
jeshi la Algeria.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment