Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imepanga kujenga bwawa
litakalokuwa kubwa zaidi duniani itakapofika mwaka 2015. Taarifa
zinasema kuwa, bwawa hilo lilikuwa lijengwe miaka kadhaa iliyopita,
lakini ilishindikana kutokana na ukosefu wa fedha za kugharamia ujenzi
huo. Taarifa zinasema kuwa, bwawa hilo litakuwa na uwezo wa kuzalisha
umeme ambao utaweza kudhamini nusu ya mahitajio ya bara la Afrika.
Imeelezwa kuwa, bwawa hilo litakuwa na uwezo wa kuzalisha megawati
40,000 za umeme kwa saa. Taarifa kutoka Kinshasa zinasema kuwa, nusu ya
uzalishaji wa umeme huo utapelekwa nchini Afrika Kusini, kwa vile nchi
hiyo ndio mdhamini mkubwa wa ujenzi wa bwawa hilo, na umeme uliosalia
utatumika ndani ya ardhi ya Kongo na nchi nyingine za ukanda wa Maziwa
Mkuu ya Afrika.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment