Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 25 May 2013

Kongo iko tayari kwa mazungumzo na M23

                               15 Rajab,1434 Hijiriyah/ May 25,2013 Miyladiyah
 Lambert  Mende Omalanga Waziri wa Habari na Msemaji wa serikali  ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametangaza kuwa, Kinshasa  iko tayari kurejea tena kwenye  mazungumzo ya amani na kundi la waasi wa M23. Omalanga ameongeza kuwa, serikali ya Kongo iko tayari kufanya tena mazungumzo na waasi wa M23 kwa upatanishi wa serikali ya Uganda kwa shabaha ya kuandaa mazingira ya kuwapokonya silaha kwa njia za amani wanamgambo wa kundi hilo. Waziri wa Habari wa Kongo amesema kuwa, ujumbe wa serikali haujawahi kususia mazungumzo hayo, bali ujumbe wa waasi wa M23 ndio ulioondoka kwenye meza ya mazungumzo ya amani mjini Kampala.  Kwa upande wake, Amani Kabasha Msemaji wa M23 amedai  kuwa, tarehe 28 Machi mwaka 2013 serikali ya Kongo ilijiondoa  kwenye mazungumzo ya Kampala,  hatua hiyo iliandaa mazingira kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutoa azimio nambari 2098 ambalo lilisababisha kuanza tena mapigano mashariki mwa nchi hiyo.

0 comments:

Post a Comment