Wiki moja baada ya kuzikwa Seneta wa jimbo la Makueni nchini Kenya, Bw.
Mutula Kilonzo, Spika wa bunge la Seneti nchini humo, Ekwe Ethuro
ametangaza kiti hicho kuwa wazi; ikiwa na maana kwamba uchaguzi mdogo
unaweza kufanyika wakati wowote kujaza nafasi hiyo. Ethuro amesema
tayari ameiandikia barua Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC kuhusu
uamuzi huo. Tume hiyo sasa inatarajiwa kutangaza tarehe ya kufanyika
uchaguzi mdogo huko Makuweni. Mutula Kilonzo alifariki dunia majuma
matatu yaliyopita nyumbani kwake na kifo chake kimeendelea kuzusha
maswali mengi huku nadharia nyingi zikitolewa kuhusu sababu ya kifo
hicho. Timu ya madaktari walioufanyia upasuaji mwili wa Kilonzo kwa
ajili ya uchunguzi ilisema matokeo kamili yatatolewa baada ya miezi 2.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment