Mwenyekiti wa jukwaa la katiba nchini Tanzania, Deus Kibanda amesema
asasi yake inapanga kuwasilisha kesi mahakamani kuzuia mchakato wa
katiba mpya kutokana na mapungufu ambayo tume ya katiba nchini humo
imedaiwa kuyafumbia macho. Kibanda amefafanua kuwa, miongoni mwa
mapungufu yaliyopewa kisogo na Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa
na Jaji mustaafu, Joseph Warioba ni pamoja na vyama vya siasa kuteka
nyara mchakato wa mabadiliko ya katiba, wananchi kukosa kuelimishwa
barabara kuhusu mchakato huo na kukosa kuhusishwa kikamilifu wadau wa
shughuli hiyo ya kuunda katiba mpya. Hii ni katika hali ambayo, Chama
cha upinzani cha CUF kimesema kupitia mwenyekiti wake Profesa Ibrahim
Haruna Lipumba kwamba, serikali inapanga mkakati wa kuvuruga mchakato wa
kuandaa rasimu ya katiba mpya ili iweze kubakia madarakani kwa zaidi ya
muda wa miaka 5 ulioainishwa na katiba ya sasa.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment