Umoja wa Mataifa umemtangaza Jenerali Carlos Alberto dos Santos Cruz
kuwa Kamanda wa Vikosi vya Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo. Jenerali Cruz raia wa Brazil mwenye umri wa miaka
61alikuwa kamanda wa vikosi vya Umoja wa Mataifa nchini Haiti kuanzia
mwaka 2007 hadi 2009. Jenerali Cruz anachukua nafasi iliyoachwa wazi na
Luteni Jenerali Chander Prakash raia wa India ambaye amemaliza muda wake
wa miaka miwili wa kuhudumu nchini Kongo. Imeelezwa kuwa, uteuzi wa
kamanda huyo ulichelewa kidogo ili kutoa fursa kwa serikali ya Afrika
Kusini kupendekeza afisa wa ngazi za juu wa jeshi atakayechukua jukumu
hilo, lakini ilishindwa kumpata afisa wa jeshi mwenye uwezo wa
kuzungumza kwa ufasaha lugha ya Kifaransa.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment