Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 2 May 2013

Cuba yaitaka Marekani ifunge jela ya Guantanamo

Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Bruno Rodriguez Parrilla ameitaka Marekani ifunge jela iliyozusha mjadala mkubwa ya Guantanamo Bay na kukirejesha kituo hicho cha kijeshi kwa serikali ya Havana.
Parilla amesema hayo katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva na kuongeza kuwa, kuna wasiwasi mkubwa kuhusu hatua za muda mrefu na za ukiukaji wa haki za binadamu zinazochokuliwa dhidi ya mahabusi wanaoshikiliwa katika jela hiyo iliyo kwenye ardhi ya Cuba iliyoghusubiwa na Marekani. Amesema, inasikitisha kuona kuwa Guantanamo Bay kimekuwa kituo cha mateso na vifo vya wanaoshikiliwa. Matamshi hayo ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba yametolewa siku moja baada ya Rais Barack Obama wa Marekani kuahidi kufanya jitihada mpya za kufunga jela hiyo ya kijeshi. Marekani inawashikilia watu 166 huko Guantanamo Bay ambao wengi wao wamekamatwa bila kujulikana makosa yao wala kufikishwa mahakamani.

0 comments:

Post a Comment