Ban Ki-moonKatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ameonyesha wasiwasi wake
kuhusiana na mwenendo wa uchaguzi ujao nchini Madagascar. Ban amesema
hayo leo na kuongeza kuwa, Umoja wa Afrika AU na Baraza la Usalama la
Umoja wa Mataifa kwa pamoja zina wasiwasi kuhusiana na hali ya
Madagascar kuelekea uchaguzi ujao wa rais na kuitaka mirengo yote ya
kisiasa nchini humo kufanya juhudi za haraka za kuafikiana juu ya kuunda
serikali ya umoja wa kitaifa. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
amesisitiza kuwa, UN inaunga mkono mabadiliko nchini humo na kuyataka
makundi ya kisiasa kukaa kwenye meza moja ya mazungumzo. Aidha ameyataka
makundi ya kisiasa kufumbia macho baadhi ya matakwa yao ya kisiasa ili
kuiepusha serikali ya mpito iliyoko madarakani na matatizo makubwa
zaidi. Matamshi hayo yametolewa katika hali ambayo, siku ya Ijumaa Umoja
wa Afrika ulitangaza kuwa, hautamtambua Andry Rajoelina Rais wa mpito
wa Madagascar iwapo atachaguliwa kuwa rais wa nchi hiyo, kwenye uchaguzi
ujao.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment