Umoja wa Afrika umesema kuwa, hautamtambua Andry Rajoelina Rais wa mpito
wa Madagascar iwapo atachaguliwa kuwa rais wa nchi hiyo, kwenye
uchaguzi ujao wa rais. Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika
limetangaza kuwa, wale wote waliosababisha serikali na katiba
kubadilishwa nchini humo wanazuiliwa kushiriki kwenye kinyang'anyiro cha
uchaguzi huo. Baraza hilo limesema kuwa, Rajoelina aliingia madarakani
mwaka 2009, baada ya kuuangusha utawala halali wa Rais Marc Ravalomanana
kiongozi wa zamani wa nchi hiyo. Hivi karibuni Umoja wa Ulaya
ulitangaza kutowatambua viongozi wa Madagascar ambao watachaguliwa
kinyume na maagizo ya Umoja wa Afrika au Jumuiya ya Ustawi ya Kusini mwa
Afrika SADC, ambayo ndio mpatanishi wa mgogoro wa Madagasca
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment