Shirika la Afya Duniani WHO linasema
eneo la Pembe ya Afrika limekumbwa na aina mpya na hatari ya ugonjwa wa
polio kwa kifupi WPV1. Mtoto wa umri wa miezi minne aliripotiwa
kuonekana akiwa na dalili za ugonjwa huo na kulemaa karibu na kambi ya
Dadaab nchini Kenya mnamo tarehe 30 mwezi Aprili mwaka huu.
Utafiti kuhusu ugonjwa huu unaendelea.
Ili kukabiliana na mkurupuko huo kampeni ya kwanza ya utoaji wa chanjo
ikiwalenga watoto 440,000 ilianza mwezi Mei mwaka huu nchini Somalia
huku awamu ya pili ikipangwa kuanza tarehe 26 mwezi huu kwenye sehemu
zilizoathirika nchini Kenya. WHO imesema hatari kwa mataifa jirani ni ya
juu kutokana na kuhama hama kwa watu wengi kwenye Pembe Ya Afrika.
Kambi ya Dadaab iliyoko kaskazini mashariki mwa Kenya ni makao ya karibu
wakimbizi 500,000 kutoka sehemu tofauti za Pembe ya Afrika. Tahadhari
ya kutaka ufanyike utafiti imetolewa kwa nchi zote katika Pembe ya
Afrika ya kutaka vifanyiwe uchunguzi visa vyote. Mwaka 2005 ugonjwa wa
polio ulisambaa kutoka barani Afrika hadi nchini Yemen ambapo visa 700
vya ugonjwa huo viliripotiwa. Tangu wakati huo chanjo mpya za ugonjwa wa
polio zimebuniwa ambazo zitazuia mikurupuko ya ugonjwa wa polio kwa
muda mrefu.
0 comments:
Post a Comment