Watu wasiopungua 176 wameuawa na kujeruhiwa baada ya kujiri milipuko 21
ambapo 17 kati ya hiyo ilikuwa ya utegaji mabomu ndani ya magari kwenye
maeneo mbalimbali huko Baghdad mji mkuu wa Iraq. Taarifa zinasema kuwa,
watu wasiopungua 85 wameuawa na wengine wasiopungua 90 kujeruhiwa kwenye
milipuko hiyo iliyotokea ndani ya muda wa masaa mawili tu mjini
Baghdad. Milipuko hiyo imetokea katika hali ambayo, majeshi ya ardhini
na angani ya nchi hiyo siku ya Jumapili yalitekeleza oparesheni kubwa
katika mikoa ya al Anbar ulioko magharibi, Babil ulioko katikati,
Karkuk ulioko kaskazini na mkoa wa Diyala ulioko mashariki mwa Iraq na
kufanikiwa kuwaangamiza magaidi 14 na kuwakamata wengine 76.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment