Watu wasiopungua 10 wamehukumiwa adhabu ya kifungo cha kati ya miezi 18
hadi 24 jela nchini Jamhuri ya Azerbaijan baada ya kupatikana na hatia
ya kulalamikia marufuku ya uvaaji wa hijabu kwenye shule za nchi hiyo.
Mahakama ya Baku imetoa hukumu hiyo kwa watu hao waliokuwa wakipinga
marufuku iliyowekwa na serikali ya kuvaa hijabu mashuleni. Inafaa
kuashiria hapa kuwa, kundi la wananchi lilifanya maandamano makubwa
mwezi Oktoba mwaka jana mbele ya Wizara ya Elimu ya Azerbaijan,
likilalamikia marufuku ya uvaaji hijabu mashuleni na kusababisha watu
kadhaa kutiwa mbaroni baada ya askari polisi kupambana na waandamanaji
hao waliokuwa na hasira. Inafaa kuashiria hapa kuwa asilimia 99.2 ya
wananchi wa Jamhuri ya Azerbaijan ni wafuasi wa dini ya Kiislamu.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment