Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 18 April 2013

Watu 63 wafariki dunia kutokana na mafuriko Keny

Naibu Rais wa Kenya, William Ruto amesema takriban watu 63 wamefariki dunia na zaidi ya 35 000 wameachwa bila makao kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. William Ruto amesema serikali inafanya juu chini kuona walioathirika wanapata misaada haraka iwezekanavyo. Naibu rais pia ameliamuru jeshi lisaidie kufanikisha zoezi la kuwaondoa watu katika maeneo yanayoendelea kushuhudia mvua kubwa na ambayo huenda yakakumbwa na mafuriko siku chache zijazo. Ruto pia ametaka shirika la Msalaba Mwekundu kuchukua hatua za haraka ili kuwasaidia watu waliofikwa na janga hilo la kimaumbile. Idara ya hali ya hewa imetahadharisha kuwa maeneo mengine mengi ya Kenya huenda yakakumbwa na mafuriko kwani mvua zitaendelea kunyesha. Hadi sasa maeneo ya kaskazini mashariki na baadhi ya maeneo ya Pwani nchini humo ndiyo yaliyoathiriwa pakubwa na mafuriko hayo.

0 comments:

Post a Comment