Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 13 April 2013

Waislamu Ujerumani wataka Wanazi washtakiwe

 Baraza Kuu la Waislamu nchini Ujerumani limetoa wito wa kushtakiwa wafuasi wapya wa fikra za unazi nchini humo kwa tuhuma za kuwaua wahajiri kadhaa wa kigeni katika nchi hiyo. Duru za habari zinaripoti kutoka Munich Ujerumani kwamba, Aiman Mazyak Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu nchini Ujerumani ametoa wito kupandishwa kizimbani wafuasi wapya wa fikra za unazi nchini humo ambao wanatuhumiwa kuwaua wahajiri 9 wa Uturuki na Ugiriki. Aiman Mazyak amesema, Waislamu wa Ujerumani wana matumaini kwamba, kwa kuwa sheria ni msumeno basi itafanya kazi yake na wafuasi hao wa unazi kupandishwa kizimbani kujibu kesi ya mauaji. Mahakama ya Katiba ya Ujerumani jana ilitoa amri ya kuandaliwa mazingira kwa ajili ya kuweko katika ukumbi wa mahakama waandishi wa habari wa Kituruki na Kigiriki. Aiman Mazyak Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu nchini Ujerumani amesema kuwa, kuandaliwa mazingira ya kuhudhuria kesi hiyo waandishi hao wa habari isiwe sababu ya kuakhirishwa kesi hiyo.  Ikumbukwe kuwa, genge la watenda jinai nchini Ujerumani linalojulikana kwa jina la Zwickau ambalo linafuata fikra za Kinazi liliwaua wahajiri 8 wa Kituruki na Mgiriki mmoja baina ya mwaka 2000 na 2007 kwa chuki za kibaguzi.

0 comments:

Post a Comment