Uchaguzi mdogo katika Jimbo la Chambani, Pemba, unatarajia kufanyika Juni 16, mwaka huu.
Uchaguzi huo unafanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo
hilo kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Salum Hemed Hamis, kufariki
dunia Machi 28, mwaka huu.
Aidha, uchaguzi huo utaenda sambamba na wa madiwani katika Kata 26
za Halmashauri 21, kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi
kufuatia baadhi ya waliokuwa wanashikilia nafasi hizo kujiuzulu,
kufukuzwa, kuhama vyama au kufariki.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jullius Mallaba, uteuzi wa wagombea
wa kiti cha ubunge utafanyika Mei 17, mwaka huu, kwa kufuatiwa na
kampeni ambazo zitafanyika Mei 18 hadi Juni 15, mwaka huu.
Alisema uteuzi wa uchaguzi mdogo wa madiwani utafanyika Mei 14,
mwaka huu, wakati kampeni zitakuwa ni Mei 15 hadi Juni 15, mwaka huu.
Kata zitakazohusika katika uchaguzi mdogo wa Madiwani ni Stesheni
(Nachingwea), Nyampu-Lukano na Lugata (Sengerema), Genge na Tingeni
(Muheza), Ibugule (Bahi), Langiro (Mbinga), Manchila (Serengeti), Iyela
(Mbeya), Mbalamaziwa (Mufindi), Runzewe Mshariki (Bukombe) na Mianzini
(Temeke).
Nyingine ni Dalai (Kondoa), Minepa (Ulanga), Makuyuni(Monduli),
Bashnet (Babati), Kimandolu, Elerai, Kaloleni na Themi (Arusha), Iseke
(Singida), Dongobesh (Mbulu), Ng`ang`ange (Kilolo), Ifakara (Kilombero),
Msanze (Kilosa) na Mnima (Mtwara).
Salim Hemed Hamis alifariki dunia katika hospitali ya Taifa
Muhimbili alipolazwa siku moja baada ya kuanguka ghafla wakati
akishiriki katika vikao cha Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa.
0 comments:
Post a Comment