Rais Omar al Bashir wa Sudan amesema uhusiano wa nchi yake na Sudan
Kusini utarejea katika hali ya kawaida na kuanzishwa pia ushrikiano wa
mpakani kati ya nchi mbili. Al Bashir ameyasema hayo katika hotuba
aliyotoa hapo jana huko Juba, mji mkuu wa Sudan Kusini akiwa katika
safari yake ya kwanza huko tangu Julai mwaka 2011 wakati eneo la kusini
mwa Sudan lilipojitenga na nchi hiyo na kuwa taifa huru la Sudan Kusini.
“Ziara hii inaonyesha mwanzo wa ushirikiano wenye lengo la kurejesha
uhusiano katika hali ya kawaida baina ya nchi mbili”, amesema Rais wa
Sudan. Kwa upande wake Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amesema
amekubaliana na mwenzake wa Sudan kuendeleza mazungumzo ili kutatua
masuala yote yenye mzozo kati ya majirani hao wawili. Amesema baadhi ya
masuala yanahitajia majadiliano zaidi na kuongeza kuwa amekubali mwaliko
aliopewa na al Bashir wa kuitembelea Sudan hivi karibuni ambayo itakuwa
safari yake ya pili nchini humo tangu kusini mwa Sudan ilipojitenga na
Sudan. Mataifa hayo mawili yalikubaliana mwezi Machi kuanzisha tena
usafrishaji wa mafuta ya Sudan Kusini kupitia mpaka wa Sudan na kuchukua
hatua za kupunguza mvutano baina yao. Hata hivyo nchi hizo mbili bado
hazijafikia makubaliano juu ya nani ana haki ya kumiliki mkoa wa Abyei
pamoja na maeneo mengine yanayozozaniwa katika eneo la mpaka wa pamoja
wenye urefu wa kilomita 2,000…/
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment