Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 18 April 2013

Serikali ya CAR yanasa silaha zilizokuwa mafichoni

Serikali mpya ya wafanyamapinduzi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, imetangaza kuwa, imenasa aina kadhaa za silaha zilizokuwa zimedhibitiwa na wafuasi wa Rais wa zamani wa nchi hiyo Francosi Bozize. Waziri wa Mawasiliano wa serikali mpya ya Jamhuri ya Afrika ya Kati Christophe Gazam Betty ametangaza kuwa, silaha hizo zimenaswa katika eneo la Boy Rabe katika viunga vya mji mkuu Bangui. Aidha waziri huyo wa mpito amesema kuwa, mbali na silaha hizo zilizonaswa, askari wa Seleka pia wamewatia mbaroni askari wa gadi ya rais aliyepinduliwa madarakani nchini humo Francois Bozize ambaye hivi sasa anaishi uhamishoni nchini Benin. Gazam Betty ameongeza kuwa, askari wa Seleka wanaendelea na oparesheni kali ya kusaka silaha zinazodhibitiwa na wafuasi wa rais huyo wa zamani wa CAR. Hii ni katika hali ambayo hivi karibuni mamia ya wananchi wa nchi hiyo walifanya maandamano dhidi ya muungano wa waasi wa Seleka uliotwaa madaraka mwezi uliopita baada ya kuiangusha serikali ya Rais Francois Bozize.

0 comments:

Post a Comment