Akizumgumza na waandishi wa habari jana muda mfupi baada ya
kuwahoji viongozi hao, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Charles
Kenyela, alisema jeshi hilo liliwaita viongozi hao ili kupata ufafanuzi
kwa mambo ya kiuchunguzi.
Kenyela alisema wamepata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa viongozi
hao na tayari polisi wameanza kuwasaka watu ambao wanadaiwa kuwawinda
viongozi wa jukwaa hilo.
Aidha,Kenyela alisema watafanya uchunguzi wa kina ili kujua ukweli
wa jambo hilo kwa kuwa kazi ya jeshi hilo ni kulinda usalama wa raia na
mali zao.
Mapema wiki hii, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Jukwaa hilo,
Hebron Mwakagenda, alisema watu walifika ofisi hapo majira ya saa sita
mchana wakiwa na gari yenye namba za usajili T126 CCG ndipo walinzi wao
wakawatilia mashaka watu hao baada ya kuwahoji wakadai viongozi hao ni
marafiki zao.
Alisema cha kushangaza watu hao waliondoka katika mazingira ya kutatanisha bila kuaga au kuacha ujumbe wowote.
0 comments:
Post a Comment