Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imetaka kufunguliwa haraka vivuko
vya mpakani mwa Ukanda wa Gaza huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
Ekmeleddin İhsanoğlu, Katibu Mkuu wa OIC ametaka kufunguliwa haraka
vivuko vya mpakani mwa Ukanda wa Gaza na kukomeshwa sera za kuwaadhibu
raia kwa halaiki kupitia ufungaji wa makusudi na wa muda mrefu wa kivuko
cha Karam Abu Salim. Katibu Mkuu wa OIC amezitaka jumuiya za kimataifa
na taasisi za kutetea haki za binadamu ziushinikize utawala haramu wa
Israel ili uvifungue vivuko vya mpakani mwa Ukanda wa Gaza. Huku
akiashiria kuwa Israel ni utawala pekee unaotumia visingizio hewa vya
kiusalama kuhalalisha hatua yake kuwaadhibu watu kwa halaiki, Ekmeleddin
İhsanoğlu amesema suala hilo linaipa jamii ya kimataifa jukumu kubwa la
kuitaka ichukue hatua ya kukomesha ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu
unaofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa
Gaza. Inakadiriwa kuwa tangu ulipoanza mwaka huu wa 2013 hadi sasa
Ukanda wa Gaza umepata hasara ya jumla ya dola milioni 700 za kimarekani
kutokana na hatua ya utawala haramu wa Israel ya kukifunga mara kwa
mara kivuko cha Karam Abu Salim…/
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment